Monday, February 25, 2019

NAIBU KATIBU MKUU WAZAZI BARA NDG TIJA MAGOMA AHIMIZA UMOJA NA UPENDO KWA VIONGOZI NA WANACHAMA DODOMA PIA KUSHUKUKA CHINI KUIMARISHA MASHINA

Naibu Katibu Mkuu wa wazazi Bara Ndg Tija Magoma amewataka viongozi wa CCM Dodoma mjini na wana CCM kwa ujumla kushiriki katika vikao vya mashina na kuimarisha umoja na mshikamano ili kukiongezea mtaji na upendo Chama Cha Mapinduzi.

Ndg Magoma ameyasema hayo leo Dodoma wakati wa maadhimisho ya sherehe za kuzaliwa CCM kwa kuagiza viongozi wote bila kujali nafasi zao kushiriki katika vikao vya mashina na kuzidisha umoja na upendo kwa jamii tunayoiongoza.

Akiwa katika ziara pia alitembelea watoto wanaoishi ktk kijiji cha matumaini Dodoma mjini.

Akifungua mkutano huo mwenyekiti wa wazazi Mkoa wa Dodoma ndg Amanuel Mkumbo.
Amemuhakikishia naibu katibu mkuu kuwa wa Dodoma kupo shwari na salama kwa CCM na wote wanaoendelea kuingia Dodoma licha ya changamoto ndogondogo za kibinaadamu zinazozuilika na kutatulika.

No comments:

Post a Comment